Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Wilayani Babati, Mkoani Manyara, limewataka madereva wa magari ya abiria hususani daladala na hiace kuacha tabia ya kupakiza abiria kupita kiasi kwa tamaa za kujiongezea kipato na kuwataka kuacha mara moja, kwani ni kosa kwa mujibu wa sheria na kanuni za usalama barabarani pia huweza kusababisha ajali barabarani
Wito huo umetolewa na Sajenti wa Polisi (SGT) Dotto Aloyce kutoka kikosi cha Usalama Barabarani, Dawati la Elimu Usalama, Wilaya ya Babati Mkoani Manyara wakati akitoa elimu ya madhara ya chombo cha moto kubeba abiria au mizigo kupitiliza kupitia redio Revival FM iliyopo Mtaa wa Komoto Kata ya Bagara Halmashauri ya Mji wa Babati
SGT Dotto amesema Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani wilayani hapa linaendelea na operesheni barabarani na halitakuwa na muhali kwa dereva yeyote atakayekamatwa amezidisha abiria au mzigo
Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani limekuwa likitumia vyombo vya habari mbalimbali ikiwemo Redio na TV kutoa elimu za usalama barabarani ili kuzuia na kupunguza ajali
Reviewed by VISION MEDIATZBLOG
on
February 03, 2026
Rating:

No comments: