Sikuya wanawake Duniani Machi 8 2026 Mrakibu Mwandamizi wa Polisi kutoka Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi Wanawake (TPF-Net) Mkoani hapa Januari 30, 2026 amefanya kikao kazi na maafisa, wakaguzi na askari wa kike kwa lengo la kukumbushana wajibu wa kazi za kulinda raia na mali zao pamoja na kujadili namna bora ya kushiriki siku ya Mwanamke duniani ambayo huadhimishwa March 8 kila mwaka
Katika kikao hicho hicho kilifanyika ukumbi wa bwalo la maafisa wa Polisi Wilaya ya Babati Mkoa wa Manyara pamoja na mambo mengine, TPF-net Manyara mwaka huu, wameafikiana kuaadhimisha siku ya Mwanamke Duniani kwa kuwatembelea na kutoa misaada kwa watu wenye mahitaji maalum, kutoa elimu mbalimbali ikiwemo elimu ya Sheria, ndoa, mambo ya ujasiriamalia, protokali kwa askari na jamii, kuwapatia zawadi askari wa kike waliofanya vizuri ili kuwaongezea motisha katika utendaji kazi
Kila mwaka Machi 08 Jeshi la Polisi huungana na Dunia kuadhimisha siku ya Mwanamke duniani ikiwa na lengo la kutambua mchango na uwezo wa mwanamke katika kudumisha usalama na amani katika jamii
Reviewed by VISION MEDIATZBLOG
on
February 01, 2026
Rating:

No comments: