test

MISANGA ATOA ELIMU KUKABILIANA NA MVUA KUBWA ZA ELNINO 2023



 *ELIMU AFYA MALEZI NA MAZINGIRA* 


Tahadhari ya Mvua Kubwa kupita kiwango ( ELNINO) , kuanzia October 2023


Lazima kuchukuwa tahadhari mapema kwa kuhakikisha njia za maji ni safi na hakuna uchafu unao zuia maji kupita


Tusafishe mitaro ya maji na kuchoma taka zote na kama kuna majani ama miti katika mitaro ya maji yaondolewe yote


Tuhahikikishe taka zote zinapelekwa  katika madampu kuu  ya taka ya miji yetu. 


madampu yaliopo katika makazi ,soko , mjini n.k. taka zisikae kwa muda mrefu haraka  haraka yatolewe na kupelekwa  dampu kuu ili kuepuka  magonjwa ya mlipuko kama cholera , kichocho n.k ..mvua zitakapo anza kunyesha na kuozesha taka katika makazi ya watu na maeneo yanayo wazunguka ndo huchochea magonjwa ya mlipuko


Hakikisha mitaro ya nyumbani kwako ni safi na weka mazingira yako ya nyumbani  safi na salama kwa kukata majaini 


Tutumie fursah katika kipindi hiki  cha  mvua kwa kupanda miti zaidi katika maeneo yanayo tuzunguka na pia kufanya kazi ya kilimo 


Utunzaji wa mazingira  na usafi wa maeneo yetu  ni jukumu letu sote tutunze mazingira yatutunze .


Imetolewa na 

Ndg. Ahmed Misanga 

Mjumbe kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi -Mkoa wa Singida

MISANGA ATOA ELIMU KUKABILIANA NA MVUA KUBWA ZA ELNINO 2023 MISANGA ATOA ELIMU KUKABILIANA NA MVUA KUBWA ZA ELNINO 2023 Reviewed by VISIONMEDIA on September 11, 2023 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.