Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama barabarani Wilaya ya Babati Mkoani Manyara, katika kusherehekea siku ya Valentine Februari 14, 2026, limegawa zawadi za Valentine na kuwataka madereva wa vyombo vya moto wilayani hapa kuonesha upendo kwa abiria na watumiaji wengine wa Barabara kwa kuzingatia na kufuata sheria za Usalama Barabarani ili kukinga na ajali zinazoweza kuepukika
Wito huo umetolewa na Mrakibu wa Polisi (SP) Emmanuel Kandola na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Wilaya ya Babati (DTO) Mkoa wa Manyara akiwa ameambatana na Sajenti wa Polisi Veronica pamona na SGT Isaya kutoka kikosi cha Usalama Barabarani ambapo amewataka madereva kuadhimisha siku ya Valentine kwa kuonyesha upendo abiria wao kwa kuendesha kwa uangalifu vyombo vyao vya moto kwa lengo la kupunguza ajali na kulinda Maisha pamoja na kujenga jamii salama
"Valentine hii chagua upendo, chagua Usalama Barabarani, Mpendwa wako anakusubiri urudi salama" amemalizia DTO SP Kandola
Reviewed by VISION MEDIATZBLOG
on
February 15, 2026
Rating:

No comments: