Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe Regina Ndege Qwaray ametoa viti,45 kompyuta/ laptop 36 kabati, na meza kwa shule za msingi Sekondari, zahanati na vituo vya Afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati
Akizungumza kwenye Hafla fupi ya ugawaji vifaa hivyo leo katika Makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Babati Mhe Qwaray amesema vifaa hivyo amevipata kutoka kwenye Taasisi mbalimbali na kuona uhitaji katika shule , zahanati , vituo vya Afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati.
Wakati huo huo Mhe Qwaray amepata fursa ya kuongea na Watumishi ambapo amewapongeza Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Babati kwa kujituma kufanya kazi na kutatua changamoto za Wananchi.
Aidha Mhe Qwaray amesisitiza Watumishi hao kujenga mahusiano mazuri kati yao na Watumishi wengine na wananchi ujumla ili kujiletea maendeleo huku akisisitiza Watumishi kuithamini na kupenda kufanya kazi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mhe John Noya na Mkurugenzi Mtendaji Anna Mbogo wameshukuru kwa msaada huo na kuomba ushirikiano huo uendelee.
Reviewed by VISION MEDIATZBLOG
on
June 12, 2026
Rating:



No comments: