Baraza la madiwani halmashauri ya wilaya ya Babati limejadili rasmi ya mpango na bajeti kwa mwaka fedha 2026/2027 na kugusa sekta mbali mbali.
Katika baraza hilo mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Babati John Noya amewataka madiwani kuhakikisha wanasimamia miradi iliyoko kwenye kata zao kwa kuwa ni wawakilishi wa wananchi
Noya amesema bajeti ya vituo vyote vya afya katika halmashauri ya wilaya ya Babati ni zaidi ya shilini millioni 655.
kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Babati Anna Mbogo amewataka madiwani kufanya uhamasishaji wa makusanyo ya mapato ya ndani.
Awali baadhi ya madiwani wamelalamikikia changamoto ya magari kutopita maeneo ya stendi ikiwemo stendi ya Dareda na kupelekea kupoteza mapato ya ndani.
BARAZA LA MADIWANI BABATI DC WAANZA KUJADILI MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2026-2027
Reviewed by VISION MEDIATZBLOG
on
February 17, 2026
Rating:
Reviewed by VISION MEDIATZBLOG
on
February 17, 2026
Rating:






No comments: