Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Emmanuela Kaganda na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Babati Anna Mbogo wamepongeza Wadau wa maendeleo walioko katika H/ Wilaya ya Babati kwa kushirikiana na Serikali katika kuwaletea Wananchi maendeleo . Viongozi hao wameyasema hayo leo kwenye Kikao maalum cha kamati ya ushauri ya Wilaya (DCC) cha kujadili mapendekezo ya Mpango na Bajeti ya Halmashauri ya Wilaya kwa mwaka 2026/2027 kilichofanyika katika katika Ukumbi wa Halmashauri ambapo Halmashauri Wilaya ya Babati. TARURA, RUWASA , BAWASA , Shirika Karimu Foundati na So They Can (STC) wamewasilsha mipango na Bajet zao. "Tunawashukuru sana wadau wote wa maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya kwa kushirikiana na Serikali kuwaletea Wananchi maendeleo wamesisitiza viongozi hao. Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji Anna Mbogo ameomba wadau hao kuweka mpango wa kujenga Madarasa ya kidato cha kwanza kwa ajili ya mapokezi ya wanafunzi Kwa mwaka 2028 ambapo wanafunzi walipo sasa darasa la Sita na walioko darasa la Tano mwaka huu wote kwa pamoja watakutana Kidato Cha kwanza mwaka 2028.
Wakati huo huo Mhe. Kaganda amesisitiza TARURA wanapotengeneza Barabara kuhakikisha wanatengeneza mitaro ya maji na kushughulikia maeneo yote korofi kwenye Barabara.
Kwa upande wa RUWASA na BAWASA , Mhe Kaganda amewasisitiza wanapojenga miradi ya maji wahakikishe maji yanafikishwa kwenye Taasisi Umma mf shule hospital na vituo vya Afya.. Kikao Cha kamati ya Ushauri Wilaya kimehudhuriwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama, Viongozi wa Vyama vya siasa, Watendaji na wataalamu Kutoka Taasisi , Idara na wakala wa Serikali zilizomo katika Hamshauri ya Wilaya ya Babati.
Reviewed by VISION MEDIATZBLOG
on
February 07, 2026
Rating:


No comments: