Babati. Manyara
Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara limeitaka jamii mkoani humo kuendelea kufichuwa viashiria vya Uhalifu na watu wenye mienendo ya kutiliwa shaka ili wachukuliwe hatua kwani jamii sio mtazamaji wa uhalifu bali ni mshiriki muhimu sana katika kuubaini, kuuzuia na kuutanzua katika jamii
Wito huo wa Ushirikishwaji jamii umetolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ahmed Makarani ofisini kwake wakati akielezea namna Ushirikishwaji jamii unavyozuia uhalifu na wahalifu Mkoani hapa
" Ushirikiano kati ya jamii na Polisi ni nguzo muhimu ya amani na usalama. Bila ushirikiano huo, kudhibiti uhalifu huwa vigumu" amesema Makarani
Itakumbukwa kuwa jamii kushirikiana na polisi
Kutapunguza uhalifu kwa
Jamii kutoa taarifa mapema kuhusu wahalifu au vitendo vinavyotia shaka na polisi huchukua hatua kabla ya madhara kutokea
SACP Makarani amesema Ushirikiano wa Polisi na Jamii kunaimarisha amani na utulivu katika jamii na kutoa fursa ya jamii kujishughulisha katika shughuli za kiuchumi na kijamii kwa maendeleo yao na Taifa kwa ujumla
Ifahamike kwamba Jamii yeyote salama hujengwa kwa ushirikiano, mawasiliano na uaminifu kati ya wananchi na polisi.
"Polisi bila jamii hawawezi kufanikiwa, na jamii bila polisi haiwezi kuwa salama" Amesisitiza Makarani
Reviewed by VISION MEDIATZBLOG
on
February 04, 2026
Rating:

No comments: